Simba Waendeleza Kichapo baada ya kuwacharaza Toto African's Bao 3 - 0 Leo Katika Uwanja wa Uhuru

Mchezo wa simba dhidi ya Toto african's umeisha rasmi katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam, Toto wakilazwa mara tatu dhidi ya wapinzani wao simba.

Simba wamemiliki mpira muda mwingi na kupiga pasi zenye mafaniko ambo ziliwapelekea kuibuka na ushindi mzuri wa goal 3 kwa bila dhidi ya Tota African's ambao walihindwa kabisa kuliona lango la Simba.

Simba walibahatika kupiga kona nyingi ambazo zilikuwa katika haraka za kumchungilia mlinda mlango wa toto. Ata hivyo Toto walikuwa wanajaribu kuwatafuta simba ambapo katika dakika ya 10 Waziri Jr. alipata pasi nzuri na kumchungulia mlinda mlango wa simba lakini ilikuwa tayari Offside, dakika ya 16 walipata faulo nje kidogo ya eneo la 18 la simba baada ya kucheza vzuri,Toto walifanya shambulizi kali katika dakika ya 27 kupia mshambuliaji wao Lusajo lakini akashindwa kumalizia mbele ya lango la Simba.
Simba nao hawakuwa mbali na lango la Toto na hivyo kupelekea mashambulizi mengi zaidi na kona nyingi zaidi lakini katika dakika 43 Simba walipata goli la kwanza kupitia mchezaji wao Mzamiru ambaye aliunganisha kwa uzuri kabisa krosi iliyopigwa na Blagnon na hivyo hadi kipindi cha kwanza kinaisha simba walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0.

Baada ya kipindi cha pili kuanza dakika chache Mchezaji wa Simba Blagnon aliumia kichwani baada ya kugongana na beki wa Toto na hivyo kupelekea mpira kusimama kwa dakika kadhaa kabla ya Blagnon kutoka dakika ya 49 na Mavugo kuchukua nafasi yake baada ya kuumia na dakika 3 baada ya kuingia Mavugo anaindikia SIMBA bao la pili baada ya kumalizia vizuri pasi ya Mohammed. Simba walimiliki mpira kwa uzuri kabisa na kufanya mabailiko kadhaa kama kutoka kwa Mwinyi Kazimoto na nafasi yake kuchukuliwa na Jamal Mnyate  na mpira uliendelea wakati lango la Toto likishambuliwa sana na dakika ya 74 Kona iliyopigwa na Kichuya inazaa matunda baada ya kumaliziwa kwa shuti kali kutoka kwa Mzamiru na hivyo kufanya Simba kuwa mbele kwa mabao 3.
Mashambulizi yaliendelea mpaka mwamuzi alipopuliza kipenga kuashiria mpira umekwisha na Simba wakiongoza kwa mabao matatu yaliyafungwa na Mzamiru 2 na Mavugo 1 wakati wapinzani wao (Toto) wakiwa awajapata kuona lango la Simba.

Mechi nyingine zilizochezwa ni
 
Msimamo wa Vodacom Premier league baada ya mechi za leo ni kama ifuatavyo:-
 

Powered by Blogger.