EPL: Mourinho aondoka darajani kwa kichapo kikali cha bao 4 - 0

Chelsea Vs Manchester United 4-0: Uwanjani Stamford Bridge kwenye Ligi Kuu England, ambayo ni mechi ya kwanza Jose Mourinho kurejea uwanjani hapo tangu afukuzwe Umeneja Chelsea Desemba 2015.

Man U, wakionyesha kusuasua katika game ya leo, walikuwa nyuma 2-0 hadi mapumziko na Chelsea walipata bao lao la kwanza dakika ya kwanza, sekunde ya 34 tu kupitia Pedro.
Bao la Pili la Chelsea lilifungwa na Gary Cahill.

Kipindi cha pili, Chelsea waliongeza bao nyingine 2 kaika dakika ya 62 na 70 wafungaji wakiwa Hazard na Kante.

Matokeo haya yamewaweka Chelsea nafasi ya 4 wakati Man United wanabaki nafasi ya 7.

Vikosi.
Chelsea:
Courtois; Azpilicueta, David Luiz, Cahill; Moses, Kante, Matic, Alonso; Pedro [Chalobah, 71’], Hazard [Willian, 78’] Diego Costa [Batshuayi, 78’]

Sub: Begovic, Aina, Terry, Chalobah, Oscar, Willian, Batshuayi.

Manchester United:
De Gea; Valencia, Bailly [Rojo, 52’], Smalling, Blind; Herrera, Fellaini [Mata, 45’], Lingard [Martial, 65’], Pogba, Rashford, Ibrahimovic.

Sub: Romero, Rojo, Darmian, Carrick, Young, Mata, Martial.

Refa: Martin Atkinson
Powered by Blogger.